Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo (Mb) amezindua Miongozo ya Uzalishaji Endelevu wa Mazao ya Ufuta na Jamii ya Mikunde tarehe 12 Desemba 2025 mkoani Lindi na kuwataka Maafisa Ugani na Maafisa Ushirika kutoa elimu kwa wakulima ili kuongeza uzalishaji wenye tija na kufikia masoko kwa faida. Miongozo hiyo ni ya mazao ya Choroko, Mbaazi, Maharage, Soya na Ufuta.