Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo anayesimamia Maendeleo ya Mazao na Usalama wa Chakula, Prof. Peter L. M. Msoffe, ameitaka Menejiment ya Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC) kuongeza kiwango cha upatikanaji wa mbolea nchini ili kumwezesha mkulima kufanya shughuli za kilimo wakati wote wa msimu.
Prof. Msoffe ameeleza hayo tarehe 20 Aprili 2026, jijini Dad es Salaam na kuongeza kuwa usalama wa chakula ni suala muhimu kwa nchi yetu, hivyo TFC ina jukumu la kuhakikisha mbolea inapatikana kwa wakulima wakati wote wa uzalishaji wa mazao.